Wednesday, January 27, 2016

KAMPUNI YA MAGARI YA ALLIANCE AUTOS WAFANYA MAONYESHO NDANI YA JENGO LA GOLDEN JUBILEE TOWER (PSPF)

DSC_1573
Gari aina ya Amarok Pick up ikiwa katika maonyesho ya mauzo ndani ya jengo la Golden Jubilee Towers ambapo maonyesho hayo ambayo yanaenda sambamba na uuzwaji wa magari hayo yanaendelea hadi hapo kesho jioni kwa 'showroom' hiyo. (Picha zote na Andrew Chale, modewjiblog).
DSC_1562
Amarok Pick up inavyoonekana kwa ubavuni..
DSC_1563
Amarok Pick up inavyoonekana upande wa nyuma..
DSC_1566
Gari aina ya Touareg ambayo katika 'showroom' hiyo ya jengo la Jubilee Towers jijini Dar es Salaam kama inavyoonekana.
Kwa mujibu wa Meneja Masoko wa kampuni ya magari ya Alliance Autos, ambao ni wauzaji wa magari ya Volkswagen Tanzania (VW), Sheikha Said amebainisha kuwa, maonyesho hayo ya magari na mauzo yaliyoanza jana 26 Januari, yanatarajiwa kufikia tamati siku ya kesho 28 katika jengo hilo la Golden Jubilee Towers.
"Magari yaliyo kwenye 'showroom' hii ya ndani ya jengo la Golden Jubilee Towers ni pamoja na Amarok Pick up na Touareg. Tumeyaleta karibu zaidi na wateja wetu wapate kuyaona na kujua uhalisia wa 'German Engineering'. Na pia waweze kujibiwa maswali yao yote yanayowatatiza, kujua uwezo wa VW katika barabara zote" ameeleza Meneja masoko huyo.

No comments:

Post a Comment

SEIF SHARIFF HAMAD AKIRI KUWA YEYE NI BABU KIZEE.

Seif Shariff Hamad Seif Shariff Hamad KWA mara ya kwanza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Seif Shariff Hamad amek...