Thursday, December 31, 2015

Harusi ya Bw. Godfrey Kihengu na Bi. Mariam Baraka

Mchungaji Kiongozi wa Jimbo la Tarime Samweli Nyageswa akiwafungisha ndoa Bi.Mariam Baraka Binagi (wa pili kulia) wa Rebu Tarime, Mara pamoja na Mwalimu Godfrey Godwin Kihengu (wa pili kushoto) wa Nyansurura Tarime, Mara ikiwa ni katika ibada iliyofanyika jana Desemba 30,2015 katika Kanisa Anglikana Buhemba Wilaya ya Tarime Mkoani Mara.

Mchungaji Kiongozi wa Jimbo la Tarime Samweli Nyageswa akimkabidhi bwana harusi cheti cha ndoa
Mchungaji Kiongozi wa Jimbo la Tarime Samweli Nyageswa akimkabidhi bibi harusi cheti cha ndoa
Maharusi wakionyesha vyeti vyao vya ndoa
Bi.Mariam Baraka Binagi (Kushoto) akiwa pamoja na bwana harusi Godfrey Godwin Kihengu.
Bibi harusi akimlisha keki bwana harusi
Maharusi wakinyweshana Shampeni
Maharusi Wakiwa katika picha ya pamoja na Wachungaji
Maharusi Wakiwa katika picha ya pamoja na Wazazi wake akiwemo mama yake mzazi pembeni ya bibi harusi
Maharusi Wakiwa katika picha ya pamoja na Wazazi wake
Maharusi wakiwa pamoja na Wakwe zake
Maharusi wakiwa katika picha ya pamoja na wadogo zao
Bibi harusi akiingia Ukumbini siku ya Sendoff iliyofanyika juzi Desemba 29,2015
Kushoto ni bi harusi akiwa ukumbini siku ya Sendoff iliyofanyika juzi Desemba 29,2015
Bi.Mariam Baraka Binagi (Kulia) akiwa pamoja na bwana harusi Godfrey Godwin Kihengu (Kushoto)
Kaka wa bibi harusi ambae pia ndie mmiliki wa BMG (Kushoto) akiwa pamoja na Mama Mzazi wa bibi harusi
Kaka wa bibi harusi ambae pia ndie mmiliki wa BMG (Kulia) akiwa pamoja na dada wa bibi harusi
"Tunawatakiwa Maisha Mema na Yenye Fanaka katika ndoa yenu na Mola azidi kuibariki"
Zaidi

Kampuni ya TTCL Yatoa Zawadi ya Mwaka Mpya kwa Vituo vya Yatima Dar


Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Nicodemus Thomas (kushoto) kwa niaba ya Ofisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Dk. Kamugisha Kazaura akikabidhi sehemu ya msaada kwa baadhi ya watoto kutoka Kituo cha kulelea watoto wanaoishi katika mazingira magumu cha Kiwohede kilichopo Buguruni Malapa cha jijini Dar es Salaam. Msaada huo umetolewa leo na Kampuni ya TTCL kwa ajili ya Siku Kuu ya Mwaka Mpya 2016. 

Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Nicodemus Thomas (kushoto) kwa niaba ya Ofisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Dk. Kamugisha Kazaura akimkabidhi Mlezi wa Watoto na Vijana, Stella Mwambenja wa Kituo cha kulelea watoto wanaoishi katika mazingira magumu cha Kiwohede kilichopo Buguruni Malapa cha jijini Dar es Salaam. Wengine ni baadhi ya watoto wa kituo hicho.
Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Nicodemus Thomas (kushoto) kwa niaba ya Ofisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Dk. Kamugisha Kazaura akizungumza na wanahabari mara baada ya kukabidhi sehemu ya msaada wa chakula kwa ajili ya Siku Kuu ya Mwaka Mpya 2016 kwa vituo vitatu vya watoto yatima  Dar es Salaam. Kulia ni Mlezi wa Watoto na Vijana wa Kituo cha kulelea watoto wanaoishi katika mazingira magumu cha Kiwohede, Stella Mwambenja. 
Mmoja wa watoto kutoka Kituo cha kulelea watoto wanaoishi katika mazingira magumu cha Kiwohede cha Buguruni Malapa Dar es Salaam akitoa shukrani kwa kampuni ya TTCL baada ya kukabidhiwa msaada huo na Kampuni ya TTCL kwa ajili ya Siku Kuu ya Mwaka Mpya 2016. 
Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Nicodemus Thomas (kushoto) na Ofisa Uhusiano wa kampuni hiyo, Amanda Luhanga (kulia) wakipewa historia fupi ya Kituo cha Makazi ya Wazee Nunge kwa Ofisa Mfawidhi, Ojuku Mgezi (katikati) kabla ya kukabidhi msaada wa vyakula kwa ajili ya Siku Kuu ya Mwaka Mpya.
Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Nicodemus Thomas (kushoto) akimkabidhi sehemu ya msaada wa vyakula Ofisa Mfawidhi wa Kituo cha Makazi ya Wazee Nunge, Ojuku Mgezi (wa pili kushoto) msaada huo umetolewa leo na TTCL kwa ajili ya Siku Kuu ya Mwaka Mpya 2016. Wengine ni viongozi na wawakilishi wa jumuiya ya Kituo cha Makazi ya Wazee Nunge.
Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Nicodemus Thomas (kushoto) akimkabidhi sehemu ya msaada wa vyakula Ofisa Mfawidhi wa Kituo cha Makazi ya Wazee Nunge, Ojuku Mgezi (wa pili kushoto) msaada huo umetolewa leo na TTCL kwa ajili ya Siku Kuu ya Mwaka Mpya 2016. Wengine ni viongozi na wawakilishi wa jumuiya ya Kituo cha Makazi ya Wazee Nunge.
Sehemu ya makazi ya Kituo cha Makazi ya Wazee Nunge
Sehemu ya msaada ukishushwa kwenye Kituo cha Makazi ya Wazee Nunge. Msaada huo umetolewa leo na TTCL kwa ajili ya Siku Kuu ya Mwaka Mpya 2016. Msaada huo umetolewa leo na TTCL kwa ajili ya Siku Kuu ya Mwaka Mpya 2016. 

Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Nicodemus Thomas  (kulia) akizungumza na watoto wa Kituo cha Kulelea Watoto Wanaoishi katika Mazingira Magumu cha Honoratha cha Temeke jijini Dar es Salaam leo kwa ajili ya Siku Kuu ya Mwaka Mpya 2016. 
Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Nicodemus Thomas (kulia) akimkabidhi sehemu ya msaada Mlezi wa Kituo cha Kulelea Watoto Wanaoishi katika Mazingira Magumu cha Honoratha cha Temeke jijini Dar es Salaam leo kwa ajili ya Siku Kuu ya Mwaka Mpya 2016. TTCL imetoa msaada wa mifuko ya Unga, Sukari, Mchele, Maharage na Mafuta ya Kupikia kwa vituo vitatu tofauti vya watoto wanaoishi katika mazingira magumu. 
Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Nicodemus Thomas (katikati)  kwa niaba ya Ofisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Dk. Kamugisha Kazaura akimkabidhi mmoja wa wawakilishi wa Kituo cha Kulelea Watoto Wanaoishi katika Mazingira Magumu cha Temeke cha jijini Dar es Salaam. Msaada huo umetolewa leo na TTCL kwa ajili ya Siku Kuu ya Mwaka Mpya 2016. 

Wednesday, December 23, 2015

TTCL Yazinduwa Teknolojia ya 4G LTE, Ina Kasi ya Ajabu...!

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu nchini Tanzania (TTCL), Dk. Kamugisha Kazaura (kushoto) na Ofisa Ufundi (IT) wa kampuni hiyo, Rehema Maswanya (kulia) kwa pamoja wakifungua pazia kuashiria uzinduzi wa teknolojia ya 4G LTE iliyozinduliwa leo jijini Dar es Salaam.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu nchini Tanzania (TTCL), Dk. Kamugisha Kazaura (kulia) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya uzinduzi wa teknolojia ya 4G LTE inayotolewa na kampuni hiyo. Kushoto ni Ofisa Mkuu wa Mauzo na Masoko wa Kampuni ya TTCL, Peter Ngota akiwa katika mkutano huo.
Ofisa Mkuu wa Mauzo na Masoko wa Kampuni ya TTCL, Peter Ngota (kushoto) akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) katika hafla ya TTCL kuzinduwa teknolojia ya 4G LTE iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam. Kulia ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu nchini Tanzania (TTCL), Dk. Kamugisha Kazaura.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu nchini Tanzania (TTCL), Dk. Kamugisha Kazaura (kushoto) na Ofisa Ufundi (IT) wa kampuni hiyo, Rehema Maswanya (kulia) kwa pamoja wakifungua pazia kuashiria uzinduzi wa teknolojia ya 4G LTE iliyozinduliwa leo jijini Dar es Salaam.
Uzinduzi wa mtandao unaotumia teknolojia ya 4G LTE toka TTCL leo.
Kulia ni wataalamu wa huduma ya teknolojia ya 4G LTE kutoka TTCL wakitoa ufafanuzi kwa baadhi ya wageni waalikwa walioshiriki katika hafla ya uzinduzi wa mtandao unaotumia teknolojia ya 4G LTE.
Kulia ni wataalamu wa huduma ya teknolojia ya 4G LTE kutoka TTCL wakitoa ufafanuzi kwa baadhi ya wageni waalikwa walioshiriki katika hafla ya uzinduzi wa mtandao unaotumia teknolojia ya 4G LTE.

Kushoto ni wataalamu wa huduma ya teknolojia ya 4G LTE kutoka TTCL na maofisa waandamizi wakitoa ufafanuzi kwa baadhi ya wageni waalikwa walioshiriki katika hafla ya uzinduzi wa mtandao unaotumia teknolojia ya 4G LTE


KAMPUNI ya Simu nchini Tanzania (TTCL) leo imezinduwa mtandao unaotumia teknolojia ya 4G LTE unaoanza kutoa huduma jijini Dar es Salaam. Mtandao huo wenye teknolojia mpya na ya kisasa wenye kasi kubwa utatoa huduma katika maeneo 11 ambayo ni pamoja na Uwanja wa Ndege wa Mwalimu J.K. Nyerere, Pugu Road, Posta Mpya, Upanga, Kinondoni, Ubungo, Oysterbay, Mwenge, Mbezi Tangibovu, Mbezi Exchange, Kunduchi Salasala, na Wazi Tegeta.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati akizinduwa rasmi teknolojia hiyo, Ofisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Dk. Kamugisha Kazaura alisema licha ya kuzinduwa huduma hiyo katika maeneo 11 kwa sasa mafundi wa kampuni hiyo wapo kazini wakiendelea na awamu ya pili ya kufunga mitambo ili huduma hiyo itolewe pia katika maeneo mengine 14 ya jiji la Dar es Salaam.

Aliyataja maeneo mengine ambayo mitambo inaendelea kufungwa kwa sasa kuwa ni pamoja na Kigamboni, Masaki, Temeke, Kimara, Jangwani, Kariakoo, Chuo Kikuu, Kurasini, Mbezi Chini Gongo la Mboto, Tabata, Kibamba, Kongowe na Bunju.

"...Awamu ya pili ya mradi huu itakuwa imekamilisha maeneo yaliyobaki ya mkoa wa Dar es Salaam na pia kupeleka mawasiliano hayo katika mikoa mingine ikiwa ni pamoja na Arusha, Mwanza, Mbeya, Dodoma na kwingineko," alisema Ofisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Dk. Kazaura.

Alisema uzinduzi wa teknolojia ya 4G LTE unakuwa umekamilisha nia ya siku nyingi ya kampuni ya TTCL ya kuwahudumia wateja katika nyanja zote za mawasiliano (Fixed-mobile convergence) kwa kutumia teknolojia ya simu za mezani na simu za mkononi.

Akifafanua zaidi Dk. Kazaura alisema uzinduzi wa teknolojia ya 4G LTE utakuwa na mchango mkubwa katika kukuza na kuongeza kasi ya shughuli za maendeleo ya kijamii na kiuchumi, kuchangia katika kukuza teknolojia ya habari na mawasiliano na pia kuongeza uzalishaji kwenye sekta mbalimbali za maendeleo.

Aidha aliongeza kuwa TTCL inaamini mtandao wa 4G LTE utafungua fursa pekee katika kukuza sekta ya elimu nchini kwa njia ya mtandao (E education). Na pia ubora wa huduma hiyo ya intaneti utatoa fursa kwa wanafunzi, wakufunzi, wataalam, wanazuoni na walimu kutumia teknolojia katika kujifunza mambo mbalimbali ya kitaaluma na nje ya taaluma.

Kwa upande wake Ofisa Mkuu wa Mauzo na Masoko wa Kampuni ya TTCL, Peter Ngota akifafanua zaidi kwa wanahabari alisema mtandao wa 4G LTE utaongeza fursa katika sekta ya afya ambapo hospitali, vituo vya afya, vyuo vya afya na wadau mbalimbali wataweza kutumia mtandao huo katika kuongeza ufanisi wa kutoa huduma bora za afya kwa wananchi tena kwa haraka zaidi.

Alisema mtandao huo pia utazinufaisha sekta nyingine za kiuchumi kama vile sekta ya biashara, viwanda, kilimo na nyinginezo. "...Wafanyabiashara na wazalishaji wa bidhaa wanahitaji mawasiliano ya uhakika katika shughuli zao. Mtandao huu wa 4G LTE utakuwa mkombozi wao na utaleta mageuzi katika kuongeza uzalishaji, kupanua wigo wa masoko ya bidhaa kwa wakulima, masoko kwa wajasiliamali, masoko kwa makampuni ndani na nje ya mipaka ya Tanzania," alisema Peter Ngota.

Hata hivyo, Ngota aliongeza kuwa uzinduzi huo unaenda sambamba na uboreshaji vifurushi rafiki vya intaneti kwa wananchi hivyo kuwaomba wananchi kuiunga mkono kampuni ya kizalendo ya TTCL katika kuboresha huduma za mawasiliano nchini.

Saturday, December 19, 2015

Benki ya NMB Plc Yaisaidia Zahanati ya Kimara Vifaa Tiba

Mganga Mfawidhi Zahanati ya Kimara, Dk. Alphoncina Mbinda (kushoto) akipokea baadhi ya mashine za kupimia mapigo ya moyo kwa mgonjwa kutoka kwa Meneja Uratibu wa NMB Plc, Thomas Kilongo. Miongoni mwa mashine zilizotolewa ni pamoja na mashine ya kupimia joto la mgonjwa, mashine 10 za kupimia 'BP' kwa mgonjwa, mashine 10 za kupimia mapigo ya moyo, mzani wa kupimia uzito na urefu kwa wagonjwa, vifaa vya kukusanyia taka, spika na kipaza sauti chake pamoja na mashine nyingine za kisasa kwa ajili ya vipimo anuai kwa wagonjwa.
Mganga Mfawidhi Zahanati ya Kimara, Dk. Alphoncina Mbinda (kushoto) akipokea baadhi ya mashine za kupimia mapigo ya moyo kwa mgonjwa kutoka kwa Meneja Uratibu wa NMB Plc, Thomas Kilongo. Miongoni mwa mashine zilizotolewa ni pamoja na mashine ya kupimia joto la mgonjwa, mashine 10 za kupimia 'BP' kwa mgonjwa, mashine 10 za kupimia mapigo ya moyo, mzani wa kupimia uzito na urefu kwa wagonjwa, vifaa vya kukusanyia taka, spika na kipaza sauti chake pamoja na mashine nyingine za kisasa kwa ajili ya vipimo anuai kwa wagonjwa.
Mganga Mfawidhi Zahanati ya Kimara, Dk. Alphoncina Mbinda (kushoto) akitoa neno la shukrani kwa Benki ya NMB Plc mara baada ya kukabidhiwa mashine mbalimbali pamoja na vifaa vya kutibia wagonjwa katika Zahanati hiyo. 
Baadhi ya maofisa wawakilishi wa Benki ya NMB Plc wakiongozwa na Meneja Uratibu wa benki hiyo, Thomas Kilongo (wa tatu kulia) wakisoma orodha ya vifaa vilivyo kabidhiwa na benki hiyo kama msaada kwa Zahanati ya Kimara.
Baadhi ya maofisa wa Benki ya NMB Plc pamoja na manesi wa Zahanati ya Kimara ya jijini Dar es Salaam wakipokea baadhi ya vifaa vya msaada vilivyotolewa na benki ya NMB Plc.
Baadhi ya maofisa wa Benki ya NMB Plc pamoja na manesi wa Zahanati ya Kimara ya jijini Dar es Salaam wakipokea baadhi ya vifaa vya msaada vilivyotolewa na benki ya NMB Plc.
Mganga Mfawidhi Zahanati ya Kimara, Dk. Alphoncina Mbinda (kushoto) akitoa neno la shukrani kwa Benki ya NMB Plc mara baada ya kukabidhiwa mashine mbalimbali pamoja na vifaa vya kutibia wagonjwa katika Zahanati hiyo.
Baadhi ya manesi wa Zahanati ya Kimara ya jijini Dar es Salaam na wafanyakazi wa NMB Plc wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kupokea msaada wa mashine mbalimbali za kuchukulia vipimo kwa wagonjwa. Vifaa hivyo vina thamani ya shilingi milioni 1.9. 
Mkuu wa kitengo cha huduma ya afya kwa mama na mtoto wa Zahanati ya Kimara ya jijini Dar es Salaam, Prosister Kiwango (wa kwanza kushoto) akitoa tangazo kwa wagonjwa kutumia spika pamoja na kipaza sauti kilichotolewa kama msaada na Benki ya NMB Plc kwa Zahanati hiyo.

Friday, December 18, 2015

Sabina Leonce Komba wa NHIF Alamba Nondo ya Pili OUT

san2
Sabina Leonce Komba ambaye ni mtumishi wa Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa (NHIF) akipozi kwa picha mara baada ya kutunukiwa Shahada yake ya pili (Masters) ya Uongozi wa Miradi aliyoipata Katika Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kwenye mahafali ya 27 ya chuo hicho yaliyofanyika Desemba 16 mwaka huu katika viwanja vya Bungo Kibaha mkoani Pwani.san3 san4
Sabina Leonce Komba ambaye ni mtumishi wa Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa NHIF akipozi kwa picha na wenzake katika mahafali hayo.
san5
Sabina Leonce Komba ambaye ni mtumishi wa Mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa NHIF pamoja na wenzake wakisubiri kuanza kwa ratiba ya mahafali hayo.

SEIF SHARIFF HAMAD AKIRI KUWA YEYE NI BABU KIZEE.

Seif Shariff Hamad Seif Shariff Hamad KWA mara ya kwanza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Seif Shariff Hamad amek...