Sunday, October 4, 2015

MAHAFALI YA KWANZA YA KIDATO CHA NNE KENYAMANYORI SEKONDARI

Afisa Elimu Sekondari katika Halmashauri ya Mji wa Tarime Mkoani Mara George Ogutu akizungumza katika Mahafali ya Kwanza ya Shule ya Sekondari Kenyamanyori iliyopo katika halmashauri hiyo.
Na:George Binagi-GB Pazzo
Ogutu alikuwa Mgeni Rasmi katika Mahafali hayo ambayo yalifanyika jana Octoba 02,2015 katika Viunga vya Shule hiyo ambayo wakati inaanza kupokea wanafunzi wanaohitimu mwaka huu ilikuwa ni shule ya Kijiji cha Kenyamanyori na ilijengwa kwa nguvu za wakazi wa kijiji hicho ambao asilimia kubwa ni wakulima na wachache wakiwa ni wafugaji kwa msaada kidogo wa wafadhiri mbalimbali.
Wanafunzi 55 wanatarajia kuhitimu kidato cha nne mwaka huu katika shule hiyo.

Kwa sasa shule hiyo inapokea wanafunzi kutoka vijiji jirani kikiwemo kijiji cha Tagota ambacho kimeungana na kijiji cha Kenyamanyori na kuwa Kata moja ya Kenyamanyori. Awali vijiji hivyo vilikuwa katika Kata moja iliyojulikana kwa jina la Kata ya Turwa ambapo ilikuwa ikijumuisha vijiji vingine vitano kabla ya kugawanywa hivi karibuni.

Ogutu aliwataka wazazi na walezi wa wanafunzi wa shule hiyo kujenga mahusiano mazuri na walimu jambo litakalosaidia kuongeza hamasa kwa waalimu katika ufundishaji. Pia aliwahimiza katika suala la kuendelea kuchangia shughuli mbalimbali za maendeleo ya shule hiyo.
Afisa Elimu Sekondari katika Halmashauri ya Mji wa Tarime Mkoani Mara George Ogutu akizungumza katika Mahafali ya Kwanza ya Shule ya Sekondari Kenyamanyori iliyopo katika halmashauri hiyo.

Mgeni Rasmi akiwa pamoja na Uongozi wa Shule ya Sekondari Kenyamanyori tayari kwa ajili ya kukabidhi vyeti kwa wahitimu wa kwanza wa kidato cha nne katika shule hiyo.
Mmoja wa wahitimu wa kidato cha nne Kenyamanyori Sekondari akipokea Cheti cha Mwanafunzi mwenye nidhamu kutoka kwa mgeni rasmi
Mmoja wa wahitimu wa kidato cha nne Kenyamanyori Sekondari akipokea Cheti kutoka kwa mgeni rasmi
Mmoja wa wahitimu wa kidato cha nne Kenyamanyori Sekondari akipokea Cheti kutoka kwa mgeni rasmi
Mmoja wa wahitimu wa kidato cha nne Kenyamanyori Sekondari akipokea Cheti kutoka kwa mgeni rasmi
Mmoja wa wahitimu wa kidato cha nne Kenyamanyori Sekondari akipokea Cheti kutoka kwa mgeni rasmi
Mmoja wa wahitimu wa kidato cha nne Kenyamanyori Sekondari akipokea Cheti kutoka kwa mgeni rasmi
Mmoja wa wahitimu wa kidato cha nne Kenyamanyori Sekondari akipokea Cheti kutoka kwa mgeni rasmi
Mwanamichezo bora akipokea cheti kutoka kwa mgeni rasmi. Bado ni mwanafunzi wa Kenyamanyori Sekondari na alikuwa mshindi wa nne kitaifa katika mashindano ya UMISSETA nchini katika mchezo wa riadha ambapo kimkoa alikuwa mwanafunzi wa kwanza.
Mwalimu wa taaluma akipokea cheti cha utambuzi kutoka kwa mgeni rasmi
Mkuu wa Shule ya Sekondari Kenyamanyori Kabengo Zacharia akipokea zawadi kutoka kwa mgeni rasmi
Wahitimu wa kidato cha nne shule ya sekondari Kenyamanyori
Wahitimu wa kidato cha nne shule ya sekondari Kenyamanyori
Wazazi na Walezi wa Wahitimu wa kidato cha nne shule ya sekondari Kenyamanyori
Wazazi na Walezi wa Wahitimu wa kidato cha nne shule ya sekondari Kenyamanyori
Wazazi na Walezi wa Wahitimu wa kidato cha nne shule ya sekondari Kenyamanyori

Wazazi na Walezi wa Wahitimu wa kidato cha nne shule ya sekondari Kenyamanyori
Picha ya Pamoja katika Mgeni Rasmi na Wahitimu wa Kidato cha nne shule ya Sekondari Kenyamanyori iliyopo Halmashauri ya Mji wa Tarime Mkoani Mara.

No comments:

Post a Comment

SEIF SHARIFF HAMAD AKIRI KUWA YEYE NI BABU KIZEE.

Seif Shariff Hamad Seif Shariff Hamad KWA mara ya kwanza Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Seif Shariff Hamad amek...